Skip to main content

WANANCHI WAHIMIZWA KUZINGATIA USAFI WA MAZINGIRA.

 

Mkuu wa Wilaya Kakonko kanali Evance Mesha Mallasa, amewataka Wananchi Wilayani Kakonko kujenga utamaduni wa kufanya usafi katika mazingira Ili kuufanya mji wa Kakonko Kuwa safi na wenye kuvutia.

Ameyasema hayo Agosti 01 2023,katika  kikao Cha maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa uhuru kilicho fanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Kakonko.


Kanali Mallasa  amewataka watumishi wa idara ya mazingira Kuwa Msatari wa Mbele kuwahamasisha wananchi kufanya usafi wa mazingira kama ambavyo viongozi wa Serikali wanasisitiza akiwamo Makamu Wa Rais Dkt Philip Isdory Mpango na vile vile kutekeleza Kwa vitendo ratiba ya kitaifa ya usafi ambapo Kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi inapaswa kutekelezwa.

Aidha amekemea,Suala La baadhi ya Watumishi wa idara ya mazingira kushindwa Kutoa ushirikiano Kwa uongozi wa Wilaya hasa pale wanapo tafutwa kwaajiri ya kupatiwa Maelekezo ya utekelezaji wa Usafi wa Mazingira.


"Viongozi kunabaadhi ya mambo tunapaswa kushirikishana,Sasa Unakuta umampigia simu Mtu wa Idara ya mazingira umshirikishe jambo la usafi wa mazingira yetu hapokei simu Wala hakutafuti hata Baada ya kuona simu Yako Wala Ujumbe mfupi hajibu pale Unapo mtumia..,niwaombe tubadilike"Alisema Kanali Mallasa.



Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli ameahidi Kufuatilia kwa karibu na kutekeleza maagizo  yaliyotolewa  kupitia idara ya mazingira Ili kuhakikisha  mji wa Kakonko unakuwa  Safi na wenye kuvutia muda Wote.

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...