Skip to main content

WANANCHI WILAYANI KAKONKO WAHIMIZWA KUTUNZA MIUNDOMBINU.

Mkuu wa Wilaya Kakonko Kanali Evance Mesha Mallasa, Leo Juni,28,2023,amewaasa Wananchi  wilayani kakonko kuitunza miundombinu mbalimbali ilinayowekwa na serikali Ili kuwahudumia Wananchi.



 Kanali Mallasa Ametoa wito Huo wakati akipokea daraja la Muda la Chuma lililojengwa katika mto Muhwazi Barabara ya Kakonko - Ikambi linalounganisha Shule ya Sekondari Ikambi na kata ya Kakonko mjini,ambalo Ujenzi wake umetekelezwa na kamandi ya Magharibi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kushirikiana na TARURA Wilaya Kakonko.



Akizungumza wakati wa kupokea daraja hilo Kanali Mallasa,Amelishukuru Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na TARURA kwa ujenzi wa daraja hilo ambalo ni kiungo muhimu kwa huduma za Jamii ikiwemo Shule ya Sekondari Ikambi.


Aidha Amewasisitiza Wananchi  Wilayani Kakonko hususani wa Kijiji Cha Itumbiko na kata nzima ya Kakonko kuitunza miundombinu ya daraja hillo Ili  iweze kudumu na kuwahudumia  Wananchi kwa ufanisi.

"Niwaombe Wananchi Pamoja na TARURA, na viongozi Wote wa kata tushirikiane kwa pamoja kulitunza daraja hili,na miundombinu hii tuitunze Ili itutunze" Alisema Kanali Mallasa.

"Hivi vyuma vilivyo jenga daraja hili ni Mali ya Jeshi,Kama ni Mali ya Jeshi Maana yake ni Mali ya serikali,uharibifu wa vyuma hivi Kwa Namna yeyote Ile itakuwa ni kuihujumu serikali inayojitahidi kuwahudumia Wananchi wake" Aliongeza Kanali Mallasa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kakonko Ndaki S.Mhuli,Ameahidi kushirikiana na Wananchi wa eneo la Itumbiko na kata ya Kakonko Kuilinda miundombinu ya daraja Ili liweze kutoa huduma Kwa Wananchi.

"Mhe.Mkuu wa Wilaya,tukuahidi,tutashirikiana na  wananchi ilikulinda miundombinu ya daraja hili ambalo limejengwa na vijana wetu wazalendo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania,Wengine tumebaki na mshangao kwani tuliamini vyuma hivi vingehitaji mashine za kuvibeba Ili viwezekufungwa lakini ni Vijana wetu hawa wazalendo kwa uchache wao wamevifunga na daraja limekamilika "aliongeza Mkurugenzi Ndaki

Daraja lililojengwa na kukabidhiwa Kwa Mkuu wa Wilaya linauwezowa kupitisha magari ya tani arobaini bila changamoto yoyote.



Daraja la Mto Muhwazi lilisombwa na maji Aprili 10,2023 kufuatia Mvua kubwa zilizonyesha na kupelekea wanafunzi   miambili (200) wa Shule ya Ikambi kushindwa kuhudhuria masomo, pamoja na Wananchi kushindwa kuvusha mazao yao toka Mashambani.

Comments

Popular posts from this blog

MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE.

 “MANENO PINGAMIZI YASIKWAMISHE UAMSHO WAKO BINAFSI” (2) Siku ya Pili 28, Aprili 2022  Semina ya Neno la Mungu - Dodoma LINK YA SOMO LA HILI YOUTUBE 👉🏼 https://youtu.be/Rwo70MEHQd0    NAMBA ZA KUTUMA SADAKA, MAOMBI NA SHUHUDA 👉🏼https://bit.ly/Sadaka-Maombi-Shuhuda  UTANGULIZI LENGO YA SOMO ➖Uamsho kutoka kwa Mungu uliokusudiwa kwa ajili yako uweze kuupata majira haya nyakati hizi. Wasomaji wa Biblia, historia ya ulimwengu na kanisa wanajua kabisa kipindi chochote kinachotangulia matatizo, kinachofuata ni maombi na baadaye unafuata uamsho. Kama kuna tatizo limepita katika taifa, ujue kuwa kuna watu watainuka kuomba kwa ajili ya lile taifa, na matokeo yake ni uamsho katika lile taifa. Hili lipo katika kanisa, familia na mahali pengine popote. Msisitizo wa somo hili ni ujue namna ya kufanya wakati Mungu anaachilia uamsho huu katika nyakati hizi, maneno pingamizi yasiwe kikwazo kwako. Pia ujue kitu cha kufanya katika kupokea uamsho huu. Uamsho unaanza na mtu bin...

GET TO KNOW WHAT IS INTERNENT

What is Internet The internet in simple terms is a network of the interlinked computer networking worldwide, which is accessible to the general public. These interconnected computers work by transmitting data through a special type of packet switching which is known as the IP or the internet protocol. Internet is such a huge network of several different interlinked networks relating to the business, government, academic, and even smaller domestic networks, therefore internet is known as the network of all the other networks. These networks enable the internet to be used for various important functions which include the several means of communications like the file transfer, the online chat and even the sharing of the documents and web sites on the WWW, or the World Wide Web. It is always mistaken said that the internet and the World Wide Web are both the same terms, or are synonymous. Actually there is a very significant difference between the t...

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...