Skip to main content

WANANCHI WILAYANI KAKONKO WAHIMIZWA KUTUNZA MIUNDOMBINU.

Mkuu wa Wilaya Kakonko Kanali Evance Mesha Mallasa, Leo Juni,28,2023,amewaasa Wananchi  wilayani kakonko kuitunza miundombinu mbalimbali ilinayowekwa na serikali Ili kuwahudumia Wananchi.



 Kanali Mallasa Ametoa wito Huo wakati akipokea daraja la Muda la Chuma lililojengwa katika mto Muhwazi Barabara ya Kakonko - Ikambi linalounganisha Shule ya Sekondari Ikambi na kata ya Kakonko mjini,ambalo Ujenzi wake umetekelezwa na kamandi ya Magharibi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kushirikiana na TARURA Wilaya Kakonko.



Akizungumza wakati wa kupokea daraja hilo Kanali Mallasa,Amelishukuru Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na TARURA kwa ujenzi wa daraja hilo ambalo ni kiungo muhimu kwa huduma za Jamii ikiwemo Shule ya Sekondari Ikambi.


Aidha Amewasisitiza Wananchi  Wilayani Kakonko hususani wa Kijiji Cha Itumbiko na kata nzima ya Kakonko kuitunza miundombinu ya daraja hillo Ili  iweze kudumu na kuwahudumia  Wananchi kwa ufanisi.

"Niwaombe Wananchi Pamoja na TARURA, na viongozi Wote wa kata tushirikiane kwa pamoja kulitunza daraja hili,na miundombinu hii tuitunze Ili itutunze" Alisema Kanali Mallasa.

"Hivi vyuma vilivyo jenga daraja hili ni Mali ya Jeshi,Kama ni Mali ya Jeshi Maana yake ni Mali ya serikali,uharibifu wa vyuma hivi Kwa Namna yeyote Ile itakuwa ni kuihujumu serikali inayojitahidi kuwahudumia Wananchi wake" Aliongeza Kanali Mallasa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kakonko Ndaki S.Mhuli,Ameahidi kushirikiana na Wananchi wa eneo la Itumbiko na kata ya Kakonko Kuilinda miundombinu ya daraja Ili liweze kutoa huduma Kwa Wananchi.

"Mhe.Mkuu wa Wilaya,tukuahidi,tutashirikiana na  wananchi ilikulinda miundombinu ya daraja hili ambalo limejengwa na vijana wetu wazalendo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania,Wengine tumebaki na mshangao kwani tuliamini vyuma hivi vingehitaji mashine za kuvibeba Ili viwezekufungwa lakini ni Vijana wetu hawa wazalendo kwa uchache wao wamevifunga na daraja limekamilika "aliongeza Mkurugenzi Ndaki

Daraja lililojengwa na kukabidhiwa Kwa Mkuu wa Wilaya linauwezowa kupitisha magari ya tani arobaini bila changamoto yoyote.



Daraja la Mto Muhwazi lilisombwa na maji Aprili 10,2023 kufuatia Mvua kubwa zilizonyesha na kupelekea wanafunzi   miambili (200) wa Shule ya Ikambi kushindwa kuhudhuria masomo, pamoja na Wananchi kushindwa kuvusha mazao yao toka Mashambani.

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...