Skip to main content

KAMATI YA SIASA YA ZURU MIRADI WILAYANI KAKONKO.


Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa Kigoma,Ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho Mkoa Kigoma Bw.Malima Mobutu, imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani Kakonko,leo Juni 30,2023.



Katika ziara hiyo ya ukaguzi wa miradi, Mkuu wa Wilaya Kakonko  Kanali Evance Mesha Mallasa,ameambatana na Kamati ya Usalama Wilaya  Kakonko, Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya Kakonko pamoja na wakuu wa idara mbali mbali kutoka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  Wilaya Kakonko.


Akizungumza Wakati wa Majumuisho ya ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM Mkoa Kigoma Bw.Mobutu ameeleza namna Kamati ya siasa ilivyoridhishwa na namna miradi hiyo inavyoendelea kutekelezwa Wilayani Kakonko,na amewataka watendaji kurekebisha kasoro ndogo ndogo zilizo bainika katika Miradi iliyotembelewa na miradi mingine Yote inayoendelea kutekelezwa.



"Kwa niaba ya Kamati ya siasa ya Chama,nitumie Fursa hii kuwapongeza watendaji wote,na kwa ujumla niseme tu,tumeridhishwa na namna miradi tuliyo tembelea inavyo endelea kutekelezwa Wilayani Kakonko" Alisema Bw.Mobutu



Aidha Amewataka wananchi Wote Wilayani Kakonko kudumisha Amani na Usalama Ili kuchochea zaidi Maendeleo.

Naye Mkuu wa Wilaya Kakonko  Kanali Mallasa, Amewataka watumishi na watendaji wote Wilayani kakonko kufanya  kazi kwa weledi Ili kuifikia adhima njema ya Mhe.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kakonko Bw.Ndaki Stefano Mhuli,ameeleza kuwa amewachukulia hatua za kinidhamu na Wengine za kisheria Ikiwamo kuwafukiza kazi watendaji waliobainika kuhusika na upotevu vifaa vya miradi ya maendeleo.



Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Bweni la Wanafunzi 120,Shule ya wasichana Kakonko Sekondari, Ujenzi wa Wodi tatu za wagonjwa Hospitali ya Wilaya Kakonko,Daraja la Chuma la Muda katika Mto Muhwazi Itumbiko, Ujenzi wa Barabara ya lami Kakonko -Itumbiko (Km 1.2),Ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Wilaya (Ikulu Ndogo),Chanzo Cha Maji Nyakayenzi pamoja na Mradi wa Stendi ya Mabasi Wilaya Kakonko, Mradi ambao  umesimama kwa muda mrefu.

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...