Skip to main content

TOENI HUDUMA KWA KUZINGATIA MAADILI-KANALI MAGWAZA




Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Aggrey John Magwaza ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kibondo ameyahimiza Mashirika yasiyo ya kiserikali kutoa huduma kwa kuzingatia misingi na maadili ya kitanzania.

Kanali Magwaza amesema hayo katika Warsha ya Mkutano wadau wa Mashirika yasiyo ya kiserikali Wilayani Kakonko iliyofanyika Mei 16, 2023, katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko.

Mkuu wa Wilaya ameeleza katika kipindi hiki yameibuka mashirika yanayounga mkono suala la ndoa za jinsia moja jambo ambalo si jema katika jamii za kiafrika, hivyo ameyasisitiza mashirika kutotekeleza shughuli hizo hata kama ni sehemu ya majukumu yao.

Aidha katika hotuba yake ameeleza anatambua mchango mkubwa unaotolewa na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na anayapongeza kwa mchango huo vile vile kuna baadhi ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali hapa nchini yamekuwa hayazingatii wajibu wao wa kisheria hivyo kusababisha malalamiko na manung’uniko kutoka kwa wananchi na baadhi ya wadau  wa maendeleo wanaotoa fedha zao kuchangia katika juhudi za nchi kujiletea maendeleo.



‘Naiagiza Halmashauri kupitia ofisi ya maendeleo ya jamii kuhakikisha mashirika yote yasiyokuwa ya kiserikali yanatekeleza shughuli zao kulingana na usajili, malengo na vipaumbele vya taifa, aidha ninayataka mashirika  yasiyokuwa ya kiserikali yajielekeze kufanya kazi maeneo yenye uhitaji ikiwemo vijiji badala ya kujikita maeneo ya mjini pekee’. Alisema kanali Aggrey Magwaza.



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko Ndaki Stephano Mhuli ameeleza mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yamekuwa na msaada mkubwa sana katika Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kwani mashirika yanafanya kazi nzuri ya kuchangia katika ujenzi wa madarasa, ujenzi wa vituo vya afya, ujenzi wa wodi ya mama na mtoto pia wamefanya shughuli ya ugawaji wa taulo kwa watoto wa kike shuleni na ugawaji wa baiskeli kwa wanafunzi wa kike wanaotembea umbali mrefu hasa wanaoishi katika mazingira magumu.

CHANZO:HALMASHAURI WILAYA KAKONKO

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...