Skip to main content

TANZANIA YAPOKEA MKOPO WA TRILIONI 1.8 TOKA BENKI YA DUNIA.

 


Serikali ya Jamuhuhuri ya Muungano wa Tanzania Kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imepokea mkopo wa Dola za Marekani Milioni 775 (tsh trilion 1.8) Kutoka Benki ya Dunia.

Taarifa Rasimi Kutoka Wizara ya Fedha na Mipango,inasema Fedha hizo za  mkopo na msaada wa masharti nafuu zimetolewa Kwa Serikali ya Tanzania kwaajiri ya kusaidia Utekelezaji wa Bajeti,Kuboresha Uchumi na Huduma za afya.

Aidha Wizara imeainisha mchanganuo wa Fedha hizo Kuwa Dola za marekani milioni 500 (Sawa na shilingi trilioni 1.1)zitatolewa na shirika la kimataifa la Maendeleo(IDA), kwa ajiri ya kufufua uchumi ulio athiriwa na mlipuko wa Ugonjwa wa UVIKO 19 pamoja na Vita  vinavyo endelea kati ya Urusi na Ukiraine.

Vile vile Dola za Marekani milioni 25 (sh.bilioni 58.1) zitatolewa kama Msaada na mfuko Wa Dunia wa kusaidia Wanawake,Vijana na watoto.

Wizara imeainisha Matumizi ya Fedha zote kuwa,Dola milioni 250(sh.Bilioni 581) Zitatumika kwaajiri ya Program ya Afya ya mama na mtoto Kwa njia ya kupima matokeo (PfoR) inayotekelezwa Tanzania Bara,na Dola za Marekani milioni 25(sh.Bilioni 58.1) Zitatumika kwaajiri ya mradi wa Uwekezaji  kiuchumi(IPF) Kwa upande wa Zanzibar.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Mwigulu Lameck Nchemba Amesema kuwa Fedha hizo zinatarajiwa kuanza kuingia nchini mapema Mwishoni mwa juma hili (Ijumaa).

Benki ya Dunia imetoa Fedha za msaada wa kibajeti ikiwa ni baada ya kipindi Cha miaka 8 iliyopita tangu Tanzania inufaike na Msaada huo.

Aidha Benki ya Dunia Pamoja na Shirika la Fedha duniani (IMF) limeipongeza Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Raisi Dkt.Samia Suluhu Hasan Kwa usimamizi wa Uchumi wake kwa uwazi na uwajibikaji Ambao umezidi kuimarika,  licha ya kuwepo athari za UVIKO 19 na Vita vya Urusi na Ukiraine. 

Vilevile Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani limezisifu Sera za kiuchumi na kifedha za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Chini ya awamu ya sita ya Raisi Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...