Skip to main content

KAMPENI NANI ZAIDI KUZINEEMESHA SIMBA NA YANGA.

 


picha chanzo @SimbaSCTanzania



Na.Anthonius Kuzenza

Timu za soka nchini Tanzania Simba na Yanga Zenye Maskani yake Jijini Dar mitaa ya Kariakoo Msimbazi na Jangwani,Zimezindua kampeni maalum Ijulikanayo Kama *_Nani zaidi_*  Yenye lengo La kuimarisha na kujenga Uwezo wa kiuchumi kwa Klabu Zote Mbili, kwa  kuwahusisha wapenzi na mashabiki Wa Timu hizo pendwa nchini Kupitia kupiga kura Huku wakichangia Kiasi Cha Tsh.1000 kwa kura Moja


Wakizungumza Mapema leo Juni 2,2022, Kupitia  Vyombo vya Habari Viongozi wa Timu Zote Mbili Wamesema kampeni hii imekuja Muda Muafaka kwani  Timu Hizi pacha zimekua Ni za Muda mrefu lakini hazijafikia mafanikio Makubwa yenye kuonekana yani kiuchumi na hata miundo mbinu licha ya mtaji wa kujizolea wapenzi na mashabiki Lukuki ndani na nje ya Nchi.Hivyo Kampeni hii itatumiwa na timu Zote kwa kuwahusisha mashabiki na wapenzi Kupiga kura Huku wakichangia Timu Zao Ili kuziwezesha kujimarisha kiuchumi.


Kampeni hii inayo simamiwa na Azam Tv Pamoja Azam pay Pamoja na Kampuni ya  Agranfore, inalenga Kizishindanisha Timu Hizi na KWA kuwahusisha wapenzi na mashabiki wake kupiga kura zitakazo wezesha  Klabu hizi pendwa ziweze kujiendesha kibiashara.


Afisa mtendaji Mkuu Wa Klabu ya Simba Barbara Gonzalezi Amesifu Kampeni  hii na Amesema  Haya.. "Kwenye mambo ya kibiashara vilabu lazima tusimame pamoja."


Gonzalez meainisha kuwa fedha zote zitakazo patikana zitaelekezwa Katika Kuboresha miundo mbinu ya Klabu na hasa uwanja "Hela zote ambazo tutapata tutapeleka kwenye ujenzi wa uwanja"Aliongeza Barbara.


Naye Afisa habari wa Klabu Ya Simba Ahamed Ally Amesema Jambo la Leo nila tofauti kidogo kwani kampeni hii ina lengo la kuziletea maendeleo  Klabu Zote mbili,Na amewahamasisha mashabiki na wapenzi wa Klabu ya Simba Kuendelea na zoezi la Uchangiaji kwani Wao walikwisha Anza hapo kabla kuchanga Ili kufanikisha ujenzi Wa miundo mbinu.


  "Nani Zaidi ni kutunishiana misuli, nani anaweza kuchangia zaidi. Ameshasema CEO fedha tunapeleka kwenye miundombinu pale Bunju. Hatuwezi kufika huko kama mashabiki hawatajitokeza kuchangia kufanikisha hili la ujenzi." alimaliza Ahamed Ally


Kwa upande Wa Klabu ya Yanga Kupitia Kaimu Afisa mtendaji Mkuu Senzo Mazingisa Mbatha,Ameeleza Kuwa Kampeni hii imekuja Wakati muafaka na inaendana na agenda iliyopo ya kuifnya Klabu ya Yanga Kuwa Klabu ya kisasa na Yenye Weledi,Hivyo inapeswa kuchukuliaa mradi huu kwa Umakini na uzito wa kipekee, lakiniAmeongeza Kuwa,Hii haimaanishi Kuwa Shughuli zingine za Klabu  zimeachwa bali Zote zinaendelea na hii Ni nyongeza ya Kati ya Shughuli nyingine zinazo endelea  ndani ya Klabu Ili kuzidi kuijenga Klabu ya Yanga.


Senzo Anasema "Hatuwezi kuchukulia mradi huu kimzahamzaha sababu,Ni Mara ya kwanza inafanyika Hapa Tanzania,Pale Timu pinzani zinakutana kujadili masuala yatakayoziwezesha kupata Fedha"


"Si Suala la mashabiki kwenda viwanjani tu na kushangilia Timu Zao Lakini Klabu Hazinufaiki na chochote" 


Amesisitiza Kuwa Ni Muda Wa Mashabiki wa Timu Zote Kupiga kura ilikuziwezesha Timu Zao kujimarisha kiuchumi.


Naye Afisa habari Yanga Haji Sundey Manara Ame wataka Mashabiki wa Yanga kupiga kura kwa Wingi Ili kuiwezesha Timu Yao kuzidi kuongoza Kama wanavyo Ongoza Kwenye Mashindano Mengine "Wanayanga Hatuna  Jambo Dogo tupige kura tuweze kushinda Kama tulivyoshinda Mechi ya tarehe ishirini na nane pale Mwanza"Alisema Manara.



Kampeni hii ya Nani Zaid itaendeshwa Kupitia mitandao ya simu Ya Vodacom,Tigo na Airtel Tanzania Ambapo watumiaji wa Mitabdao Hiyo wataingia Katika mfumo wa kifedha wa mtandao husika Ili kuwezaa kushiriki.


Kuipigia Kura Klabu ya Simba kwa watumiaji wa Vodacom namba ya Kampuni ya Ni 002233 na Namba ya kumbukumbu ni 002233,Tigo Kumbukumbu Namba 776655 na KWA Airtel Namba ya Kampuni Namba 776655 na Kumbukumbu  Namba 776655.





Kuipigia Kura Klabu ya Yanga kwa watumiaji wa Vodacom namba ya Kampuni  Ni 004455 na Namba ya kumbukumbu ni 004455,Tigo Kumbukumbu Namba 887766 na KWA Airtel Namba ya Kampuni Namba 887766 na Kumbukumbu  Namba 887766.



Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...