Skip to main content

MBOWE AJISALIMISHA POLISI


 http://www.dar24.com/wp-content/uploads/2013/07/Mbowe.jpg
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amejipeleka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ikiwa ni siku moja baada ya kundi la polisi wenye silaha za moto kuvamia nyumbani kwake kwa nia ya kumkamata.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika, jana alisema Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, aliripoti Makao Makuu ya Jeshi hilo jana saa 8:45 mchana na kuhojiwa na polisi kwa zaidi ya saa tano.
Msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso, alithibitisha Mbowe kuripoti Makao Makuu ya Polisi kwa ajili ya kuhojiwa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Mnyika, ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo (Chadema), Mbowe aliachiwa jana saa 1:45 usiku baada ya kudhaminiwa naye (Mnyika) na kwamba, ametakiwa kuripoti tena Julai 23, mwaka huu, saa 8 mchana.
Mnyika alisema Mbowe alihojiwa kwa tuhuma za uchochezi unaodaiwa kuwa unatokana na tamko alilolitoa baada ya Kamati Kuu ya Chadema kuhusisha polisi na mlipuko wa bomu uliotokea jijini Arusha.
Mlipuko huo ulitokea katika mkutano wa hadhara wa kufunga kampeni za chama hicho kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata nne za jiji hilo Juni 15 mwaka huu.
Alisema tuhuma nyingine ni madai yake kuwa polisi walipanga kukisaidia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Arusha na Rais Jakaya Kikwete na serikali kutoshiriki katika mazishi kwamba, ni ishara ya hisia za hatia kwa kuwa anatambua njama zinazopangwa na polisi dhidi ya Chadema.
Kwa mujibu wa Mnyika, katika mahojiano hayo, Mbowe alikuwa na mawakili; Peter Kibatala na Nyaronyo Kicheere.
Alisema viongozi waliomsindikiza ni pamoja na yeye (Mnyika), Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo, Benson Kigaila na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa Chadema, John Mrema.
“Tutaeleza yaliyojiri baada ya mahojiano kukamilika,” alisema Mnyika.
Juzi kundi la polisi wenye silaha za moto walivamia nyumbani kwa Mbowe, kwa nia ya kumkamata.

Kwa mujibu wa gazeti moja litokalo kila siku (siyo NIPASHE), askari hao wanaokadiriwa kufikia saba, wakiwa na silaha nzito katika gari la wazi waliwasili nyumbani kwa Mbowe majira ya saa 7:30 na kuwaamuru askari wanaolinda nyumbani kwake kumtoa Mbowe nje ili waonane naye.
Walinzi wa Mbowe walihoji uhalali wa ukamataji huo na kuwataka polisi wawaonyeshe hati ya kumkamata, lakini hawakuweza kuionyesha, hali iliyozusha wasiwasi kwa walinzi wa kiongozi huyo.
Hata hivyo, walinzi hao waliwaambia polisi hao kuwa Mbowe alikuwa safarini.
Polisi hao baada ya kuona wameshindwa kukamilisha kazi hiyo, waliwaachia walinzi hao namba ya simu ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Ernest Kimola, wakiwaagiza kuhakikisha wanamwambia Mbowe awasiliane na kamanda huyo.

Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema hawezi kuzungumza lolote kuhusiana na suala hilo kwa kuwa haliko ndani ya eneo la mipaka ya kazi yake.
Hata hivyo, alisema hakuna muda maalum uliowekwa na sheria kumkamata mtuhumiwa.

CHANZO: NIPASHE
 
 

Comments

Popular posts from this blog

MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE.

 “MANENO PINGAMIZI YASIKWAMISHE UAMSHO WAKO BINAFSI” (2) Siku ya Pili 28, Aprili 2022  Semina ya Neno la Mungu - Dodoma LINK YA SOMO LA HILI YOUTUBE 👉🏼 https://youtu.be/Rwo70MEHQd0    NAMBA ZA KUTUMA SADAKA, MAOMBI NA SHUHUDA 👉🏼https://bit.ly/Sadaka-Maombi-Shuhuda  UTANGULIZI LENGO YA SOMO ➖Uamsho kutoka kwa Mungu uliokusudiwa kwa ajili yako uweze kuupata majira haya nyakati hizi. Wasomaji wa Biblia, historia ya ulimwengu na kanisa wanajua kabisa kipindi chochote kinachotangulia matatizo, kinachofuata ni maombi na baadaye unafuata uamsho. Kama kuna tatizo limepita katika taifa, ujue kuwa kuna watu watainuka kuomba kwa ajili ya lile taifa, na matokeo yake ni uamsho katika lile taifa. Hili lipo katika kanisa, familia na mahali pengine popote. Msisitizo wa somo hili ni ujue namna ya kufanya wakati Mungu anaachilia uamsho huu katika nyakati hizi, maneno pingamizi yasiwe kikwazo kwako. Pia ujue kitu cha kufanya katika kupokea uamsho huu. Uamsho unaanza na mtu bin...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

MOST CHALLENGES FACING MARKETING MANAGER

Everyone faces problems and challenges in their jobs. And a marketing managers job has gotten tougher with more and more introduction of different media vehicles and different costs of advertising present in the market. In general, a marketing manager of the 21st century faces the following challenges. Budget allocation is a challenge for marketing managers from day one -  Where do you use your budget? Do you use it for TVC’s, hoardings, radio, online or where else? There are so many media vehicles today, and so many variant frequencies of advertising, that media planning has become a big challenge for marketers. If you select the right message but a wrong media, then the message will probably be lost. Differentiation -  The second challenge is differentiation. A customer sometimes watches 6-7 ads in a single minute. If the ads are longer, he will still watch 2-3 ads in every minute of advertisements. So how do you differentiate yourself? What is the message that ne...