Skip to main content

MBOWE AJISALIMISHA POLISI


 http://www.dar24.com/wp-content/uploads/2013/07/Mbowe.jpg
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amejipeleka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ikiwa ni siku moja baada ya kundi la polisi wenye silaha za moto kuvamia nyumbani kwake kwa nia ya kumkamata.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika, jana alisema Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, aliripoti Makao Makuu ya Jeshi hilo jana saa 8:45 mchana na kuhojiwa na polisi kwa zaidi ya saa tano.
Msemaji wa jeshi hilo, Advera Senso, alithibitisha Mbowe kuripoti Makao Makuu ya Polisi kwa ajili ya kuhojiwa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Mnyika, ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo (Chadema), Mbowe aliachiwa jana saa 1:45 usiku baada ya kudhaminiwa naye (Mnyika) na kwamba, ametakiwa kuripoti tena Julai 23, mwaka huu, saa 8 mchana.
Mnyika alisema Mbowe alihojiwa kwa tuhuma za uchochezi unaodaiwa kuwa unatokana na tamko alilolitoa baada ya Kamati Kuu ya Chadema kuhusisha polisi na mlipuko wa bomu uliotokea jijini Arusha.
Mlipuko huo ulitokea katika mkutano wa hadhara wa kufunga kampeni za chama hicho kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata nne za jiji hilo Juni 15 mwaka huu.
Alisema tuhuma nyingine ni madai yake kuwa polisi walipanga kukisaidia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Arusha na Rais Jakaya Kikwete na serikali kutoshiriki katika mazishi kwamba, ni ishara ya hisia za hatia kwa kuwa anatambua njama zinazopangwa na polisi dhidi ya Chadema.
Kwa mujibu wa Mnyika, katika mahojiano hayo, Mbowe alikuwa na mawakili; Peter Kibatala na Nyaronyo Kicheere.
Alisema viongozi waliomsindikiza ni pamoja na yeye (Mnyika), Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo, Benson Kigaila na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri wa Chadema, John Mrema.
“Tutaeleza yaliyojiri baada ya mahojiano kukamilika,” alisema Mnyika.
Juzi kundi la polisi wenye silaha za moto walivamia nyumbani kwa Mbowe, kwa nia ya kumkamata.

Kwa mujibu wa gazeti moja litokalo kila siku (siyo NIPASHE), askari hao wanaokadiriwa kufikia saba, wakiwa na silaha nzito katika gari la wazi waliwasili nyumbani kwa Mbowe majira ya saa 7:30 na kuwaamuru askari wanaolinda nyumbani kwake kumtoa Mbowe nje ili waonane naye.
Walinzi wa Mbowe walihoji uhalali wa ukamataji huo na kuwataka polisi wawaonyeshe hati ya kumkamata, lakini hawakuweza kuionyesha, hali iliyozusha wasiwasi kwa walinzi wa kiongozi huyo.
Hata hivyo, walinzi hao waliwaambia polisi hao kuwa Mbowe alikuwa safarini.
Polisi hao baada ya kuona wameshindwa kukamilisha kazi hiyo, waliwaachia walinzi hao namba ya simu ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Ernest Kimola, wakiwaagiza kuhakikisha wanamwambia Mbowe awasiliane na kamanda huyo.

Akizungumza na NIPASHE jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alisema hawezi kuzungumza lolote kuhusiana na suala hilo kwa kuwa haliko ndani ya eneo la mipaka ya kazi yake.
Hata hivyo, alisema hakuna muda maalum uliowekwa na sheria kumkamata mtuhumiwa.

CHANZO: NIPASHE
 
 

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...