Skip to main content

JELA MIAKA THELATHINI KWA KUZAA NA MWANAYE

MAHAKAMA ya Mkoa wa Mbeya imemhukumu kifungo cha Miaka 30 jela Mkazi wa Isanga Jijini Mbeya, Hamad Yusufu, kwa kosa la Kuzini na Binti yake na Kuzaa naye mtoto mmoja wa Kike.

Baba huyo anadaiwa kuanza kuzini na binti yake mwaka 2008 akiwa na umri wa miaka 11 akimtisha kwa kutumia panga na kumpa ujauzito miaka mitano baadaye na kusababisha akatishe masomo ya elimu ya msingi.


Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Gilbert Ndeuruo, amesema Mahakama imezingatia zaidi ushahidi uliotolewa na mtoto wa mshitakiwa huyo, Hadija Yusufu, anayedaiwa kuzini na kuzaa naye mtoto mmoja, Eva Yusufu, aliyethibitisha bila shaka kuwa baba yake alimlazimisha kuzini naye akimtishia kwa panga kwa zaidi ya miaka minne mfululizo kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2012, alipopata ujauzito.

Pia Hakimu Ndeuruo, amesema mahakama hiyo imeridhika bila shaka kuwa mshtakiwa Hamad amefanya kosa hilo baada ya vipimo vya vinasaba yaani DNA vilivyowasilishwa Mahakamani hapo na Afisa kutoka Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Hadija Said Mwema, kuonesha kuwa mshtakiwa huyo amefanana na mtoto Eva aliyezaliwa na binti yake Hadija, kwa asilimia 99.9.

Kwa mujibu wa taarifa zilizowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka, ulioongozwa na Mwendesha Mashtaka Lugano Mwakilasa, mshitakiwa huyo ameanza kuzini na binti yake mwaka 2008 akiwa darasa la Tano baada ya kuachana na mkewe, Regina Simon, aliyefunga naye ndoa mwaka 1997 mkoani Mbeya.

Hata hivyo, mshitakiwa huyo ameonesha nia ya kukata rufaa kupinda adhabu hiyo licha ya kushindwa kuitumia fursa ya kuomba punguzo la adhabu aliyopewa na Hakimu Ndeuruo, akidai anaiachia mahakama ifanye itakavyo kwa madai hakufanya kosa hilo bali kesi hiyo imetokana na chuki alizonazo mke wake, Regina Simon, baada ya kuachana.

Nje ya Mahakama, baadhi ya wananchi wametoa maoni yao kuhusu adhabu hiyo.

Hukumu hiyo ni ya pili kutolewa na Mahakamani hapo katika kipindi cha Julai mwaka huu kuhusu makosa ya udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya watoto wa kike, ambapo hukumu ya kwanza imetolewa na Hakimu Ndeuruo Julai Mbili mwaka dhidi ya Mchungaji wa Kanisa la Evangelical Assemblies of Gog, EAGT, mkoani Mbeya, Daniel Mwasumbi, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kumbaka na kumpa ujauzito mara mbili mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Itende mjini hapa, Neema Benson.
CHANZO STAR-TV

Comments

Popular posts from this blog

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

TISS YAPATA BOSS MPYA.

  Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amemteua Bw.Said Hussein Masoro kuwa Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa taifa,Kuchukua nafasi ya Kamishina Diwani Athuman Msuya  Ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Ikulu. Kabla ya Uteuzi huo Bw.Masoro alikua akihudumu katika Idara ya Usalama wa Taifa kama Naibu Mkurugenzi mkuu na Mkurugenzi wa shughuli za  ndani wa Usalama wa Taifa. Wakati huo huo Rais Dkt.Samia amemteua Balozi Hussein Othman Katanga Kuwa Balozi wa Tanzania mjini New York, Nchini Marekani na muwakilishi wa kudumu wa Umoja wa Mataifa. Balozi Katanga anachukia nafasi ya Balozi Profesa Kennedy Gaston,Ambaye Uteuzi wake umetenguliwa. Balozi Katanga kabla ya Uteuzi huu alikua Katibu Mkuu Kiongozi. Vile vile Mhe.Rais Dkt.Samia amemteua Bw.Moses Mpogole Kusiluka Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi,Ambapo kabla ya Uteuzi huo alikua Katibu Mkuu Ikulu. Taarifa Rasimi Kutoka Kurugenzi ya mawasiliano ya Raisi Ikulu iliyotolewa mapema Jana Januari 3,2023, i...