Skip to main content

Ripoti Maalum:Wizi wa fedha katika ATM ulivyofanyika




KUKUA kwa teknolojia za fedha ambako kumerahisisha ufanisi wa matumizi na utunzaji fedha, kunaonekana kugeuka kuwa balaa kutokana na kuibuka kwa wizi wa fedha zilizohifadhiwa kwenye akaunti za wateja.



Taarifa za wizi huu zilianza kurindima Machi 2010 na Sh300 bilioni ziliibwa kwa njia ya mtandao  kupitia mashine za ATM,   kati ya kiasi hicho Sh360 milioni zikihusisha benki moja ya NBC.
Hata hivyo, mwaka huo walikamatwa watu wanne baada ya kuripotiwa wizi huo mkubwa, sambamba na taarifa za kukamatwa kwa watu hao alikamatwa mfanyabiashara mmoja aliyefanya jaribio la kuiba  Sh221 milioni kutoka Benki ya NBC.

Wimbi la wizi huo limeibuka tena Oktoba mwaka jana hadi Februari mwaka huu, inakadiriwa Sh700 milioni zimeibwa Benki ya NMB na benki zingine kwa nyakati tofauti.

Tayari, polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB wamefanikiwa kuwatia mbaroni watu wanne ambao wanadaiwa kukutwa wakiwa kwenye mpango wa kuendelea kuiba fedha ndani ya mashine za kuchukuliwa fedha (ATM) za Benki ya NMB tawi la PPF Plaza,   saa 6:00 usiku.

Kunaswa kwa watu hao kunatokana na mtego baina ya maofisa wa benki na polisi uliofanikisha Februari 10 mwaka huu, kumtia mbaroni mtuhumiwa mmoja akiwa katika  ATM ya NMB katika tawi la PPF Plaza, akiingia kuchukua fedha ambaye alifanikisha kunaswa kwa watuhumiwa wengine na vifaa vinavyotumika kwa wizi huo.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Christopher Fuime alieleza kuwa baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo alifanikisha kukamatwa wengine, ikiwamo vifaa mbalimbali ambavyo wamekuwa wakivitumia kufanyia uhalifu huo.

“Kwa muda mrefu sasa tulikuwa tukihangaika  na wahalifu wa aina hii, kwani tangu mwaka Oktoba mwaka jana tumekuwa tukipokea kesi mbalimbali za wizi wa fedha katika akaunti zao, lakini tumefanikiwa juzi kuwatia mbaroni,” alisema.

Tangu kutiwa mbaroni kwa watuhumiwa hao, idadi ya malalamiko ambayo wastani wa kesi 15 walizokuwa wakipokea kwa siku 14 zimeisha, hali ambayo inawafanya kuamini kuwa wahusika hao walikuwa vinara wakuu wa wizi huo.

“Hatuna maana kwamba kukamatwa kwao uhalifu huu utapungua,  wizi huu una mtandao mpana kwa vile hata wahalifu hao wamedokeza wamekuwa wakifanya uhalifu huo kwa kushirikiana na wataalamu wa kompyuta kutoka nchini Bulgaria,” alisema.

Vifaa walivyokamatwa navyo
Vifaa vilivyokamatwa ni  kadi bandia za kuchukulia fedha katika ATM 194 za Banki ya NMB, kati yake kadi 95 zilikuwa na namba 0225152975 zinazotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina na picha ya mtu anayedaiwa ni mtumiaji, kadi zingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti namba 5068000322 zikitumia jina lingine na picha moja.

Pia, walinasa kadi za Benki ya DTB 36, ambazo kati yake 18 zilikuwa na jina moja la Kelvin G. Gratias zikiwa namba  20497883, kadi 12 zikitumia jina lingine na akaunti namba 2049783, huku kadi sita zikitumia jina la mtu mwingine akaunti namba 2049783.


Kadi zingine tatu zenye maandishi ya Download List na nyingine ikiwa ni kadi ya visa ya Benki ya KCB yenye namba 4183546040003827 zikitumia jina moja, kadi zingine zilikuwa ni tupu zisizo na maandishi wala nembo ya benki yoyote na nyingine zikiwa na nembo ya Soviet Royality, kadi ya raia wa Urusi ikiwa na namba Sand 000724.

Comments

Popular posts from this blog

MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE.

 “MANENO PINGAMIZI YASIKWAMISHE UAMSHO WAKO BINAFSI” (2) Siku ya Pili 28, Aprili 2022  Semina ya Neno la Mungu - Dodoma LINK YA SOMO LA HILI YOUTUBE 👉🏼 https://youtu.be/Rwo70MEHQd0    NAMBA ZA KUTUMA SADAKA, MAOMBI NA SHUHUDA 👉🏼https://bit.ly/Sadaka-Maombi-Shuhuda  UTANGULIZI LENGO YA SOMO ➖Uamsho kutoka kwa Mungu uliokusudiwa kwa ajili yako uweze kuupata majira haya nyakati hizi. Wasomaji wa Biblia, historia ya ulimwengu na kanisa wanajua kabisa kipindi chochote kinachotangulia matatizo, kinachofuata ni maombi na baadaye unafuata uamsho. Kama kuna tatizo limepita katika taifa, ujue kuwa kuna watu watainuka kuomba kwa ajili ya lile taifa, na matokeo yake ni uamsho katika lile taifa. Hili lipo katika kanisa, familia na mahali pengine popote. Msisitizo wa somo hili ni ujue namna ya kufanya wakati Mungu anaachilia uamsho huu katika nyakati hizi, maneno pingamizi yasiwe kikwazo kwako. Pia ujue kitu cha kufanya katika kupokea uamsho huu. Uamsho unaanza na mtu bin...

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

GET TO KNOW EXTENDED MARKERTING MIX

The extended marketing mix is, as the name suggests, an extension of the marketing mix which was traditionally for products. The 4P’s are also known as product marketing mix. As services came more into the picture it was seen that the 4p’s could not justify the marketing mix. There were 3 more elements which were necessary to actually explain the marketing of services. When products began offering services, the extended marketing mix began applying to products as well (like Maruti service stations where Maruti is a product and the service station is a service). These are the elements which were added to the marketing mix to form the extended marketing mix. In the above figure, the product marketing mix are the first four P’s and the next 3 P’s are added to make the Extended Marketing mix. This extended marketing mix is also known as the service marketing mix. The four PS mainly constituted the following 4 elements Product Price Place Prom...