Skip to main content

Ripoti Maalum:Wizi wa fedha katika ATM ulivyofanyika




KUKUA kwa teknolojia za fedha ambako kumerahisisha ufanisi wa matumizi na utunzaji fedha, kunaonekana kugeuka kuwa balaa kutokana na kuibuka kwa wizi wa fedha zilizohifadhiwa kwenye akaunti za wateja.



Taarifa za wizi huu zilianza kurindima Machi 2010 na Sh300 bilioni ziliibwa kwa njia ya mtandao  kupitia mashine za ATM,   kati ya kiasi hicho Sh360 milioni zikihusisha benki moja ya NBC.
Hata hivyo, mwaka huo walikamatwa watu wanne baada ya kuripotiwa wizi huo mkubwa, sambamba na taarifa za kukamatwa kwa watu hao alikamatwa mfanyabiashara mmoja aliyefanya jaribio la kuiba  Sh221 milioni kutoka Benki ya NBC.

Wimbi la wizi huo limeibuka tena Oktoba mwaka jana hadi Februari mwaka huu, inakadiriwa Sh700 milioni zimeibwa Benki ya NMB na benki zingine kwa nyakati tofauti.

Tayari, polisi mkoani Mwanza kwa kusaidiana na maofisa wa Benki ya NMB wamefanikiwa kuwatia mbaroni watu wanne ambao wanadaiwa kukutwa wakiwa kwenye mpango wa kuendelea kuiba fedha ndani ya mashine za kuchukuliwa fedha (ATM) za Benki ya NMB tawi la PPF Plaza,   saa 6:00 usiku.

Kunaswa kwa watu hao kunatokana na mtego baina ya maofisa wa benki na polisi uliofanikisha Februari 10 mwaka huu, kumtia mbaroni mtuhumiwa mmoja akiwa katika  ATM ya NMB katika tawi la PPF Plaza, akiingia kuchukua fedha ambaye alifanikisha kunaswa kwa watuhumiwa wengine na vifaa vinavyotumika kwa wizi huo.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Christopher Fuime alieleza kuwa baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo alifanikisha kukamatwa wengine, ikiwamo vifaa mbalimbali ambavyo wamekuwa wakivitumia kufanyia uhalifu huo.

“Kwa muda mrefu sasa tulikuwa tukihangaika  na wahalifu wa aina hii, kwani tangu mwaka Oktoba mwaka jana tumekuwa tukipokea kesi mbalimbali za wizi wa fedha katika akaunti zao, lakini tumefanikiwa juzi kuwatia mbaroni,” alisema.

Tangu kutiwa mbaroni kwa watuhumiwa hao, idadi ya malalamiko ambayo wastani wa kesi 15 walizokuwa wakipokea kwa siku 14 zimeisha, hali ambayo inawafanya kuamini kuwa wahusika hao walikuwa vinara wakuu wa wizi huo.

“Hatuna maana kwamba kukamatwa kwao uhalifu huu utapungua,  wizi huu una mtandao mpana kwa vile hata wahalifu hao wamedokeza wamekuwa wakifanya uhalifu huo kwa kushirikiana na wataalamu wa kompyuta kutoka nchini Bulgaria,” alisema.

Vifaa walivyokamatwa navyo
Vifaa vilivyokamatwa ni  kadi bandia za kuchukulia fedha katika ATM 194 za Banki ya NMB, kati yake kadi 95 zilikuwa na namba 0225152975 zinazotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina na picha ya mtu anayedaiwa ni mtumiaji, kadi zingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti namba 5068000322 zikitumia jina lingine na picha moja.

Pia, walinasa kadi za Benki ya DTB 36, ambazo kati yake 18 zilikuwa na jina moja la Kelvin G. Gratias zikiwa namba  20497883, kadi 12 zikitumia jina lingine na akaunti namba 2049783, huku kadi sita zikitumia jina la mtu mwingine akaunti namba 2049783.


Kadi zingine tatu zenye maandishi ya Download List na nyingine ikiwa ni kadi ya visa ya Benki ya KCB yenye namba 4183546040003827 zikitumia jina moja, kadi zingine zilikuwa ni tupu zisizo na maandishi wala nembo ya benki yoyote na nyingine zikiwa na nembo ya Soviet Royality, kadi ya raia wa Urusi ikiwa na namba Sand 000724.

Comments

Popular posts from this blog

7 BUSINESS LOCATION THAT INCREASE BRAND VISIBILITY

Marketing has changed and it has become more personal. People nowadays need convenience and you cannot expect that your customer will come to you. You will have to go to your customer again and again so that he does not switch to any other brand. Remember that your customer has numerous options in his hand. Thus your business needs to present in locations where the customer can make his buying decision easily. This is where your business location plays an important role. The process of managing a business is continually changing but more importantly with the advent of online marketing, your business location itself has changed. Because of the increasing usage of internet, Smart phones too are the latest trend and hence the reach of internet is now quadrupled. But it is not necessary that your customer be present only on the internet. Brick businesses are as alive today as online businesses. Below you will find a list of 7 business locations that you should be ...

GET TO KNOW WHAT IS INTERNENT

What is Internet The internet in simple terms is a network of the interlinked computer networking worldwide, which is accessible to the general public. These interconnected computers work by transmitting data through a special type of packet switching which is known as the IP or the internet protocol. Internet is such a huge network of several different interlinked networks relating to the business, government, academic, and even smaller domestic networks, therefore internet is known as the network of all the other networks. These networks enable the internet to be used for various important functions which include the several means of communications like the file transfer, the online chat and even the sharing of the documents and web sites on the WWW, or the World Wide Web. It is always mistaken said that the internet and the World Wide Web are both the same terms, or are synonymous. Actually there is a very significant difference between the t...

1️⃣SEMINA YA NENO LA MUNGU UWANJA WA WAJENZI-DODOMA : NA MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE

1️⃣SEMINA YA NENO LA MUNGU UWANJA WA WAJENZI-DODOMA : NA MWL. CHRISTOPHER  MWAKASEGE SIKU YA KWANZA: 27 APRILI, 2022 SOMO: “MANENO PINGAMIZI YASIKWAMISHE UAMSHO WAKO BINAFSI”  UTANGULIZI LENGO YA SOMO Uamsho kutoka kwa Mungu uliokusudiwa kwa ajili yako uweze kuupata. Na msisitizo hapa haupo kwenye maneno bali upo kwenye uamsho. Na kati ya kitu kimojawapo tutakachoshughulika nacho kwenye somo hili ni maneno pingamizi ambayo yanatafuta kila namna ya kukukwamisha ili usipokee kile Mungu alichokikusudia kwako na usifike pale Mungu alipokusudia ufike.   Na kwa leo nataka tujifunze na kuangalia juu ya UMUHIMU WA UHUSIANO WA UAMSHO WAKO WA LEO NA MAFANIKIO YAKO YA KESHO   Soma Matendo ya Mitume 12:1-17 Maandiko yanasema kwenye mstari wa 7 kusema “Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. Minyororo yake ikamwanguka mikononi.” Malaika alimwamsha Petro ili apate uamsho wake binafsi akiwa...